Kusikia kauli za nina nuksi au ana nuksi au ana mikosi ni jambo la kawaida katika jamii, kwa mtani au kwa mzaa au baada ya kuona kila jambo unalofanya linatokeza matokeo mabaya sana kiasi kwamba unakata tamaa kila kukicha na kujiuliza nina nini?
Mikosi na nuksi ni hali ya kuharibikiwa kila mara, hii inaweza kuwa ni mipango ya Mungu mmoja muumba kukuona una msimamo gani na uwezo wake, pia matatizo mengine ni sisi wenyewe tunasababisha kwa makusudi au kwa jeuri au kwa bahati mbaya.
Kuna mikosi na nuksi inavyoitwa kwa mujibu wa binadamu kukufitini hasa kwa njia za nguvu za giza maana yake uchawi na kutupiana majini.
Ukilogwa na kutupiwa majini una weza pata majanga ukayaita mikosi na nuksi.
Dalili za kulogwa au kuwa na jini au vyote viwili
- Mfano unaweza kuwa unaota mara kwa mara unalishwa vitu usingizini au
unapewa madawa na wakati mwingine unakuta asubuhi umechanjwa chale
mwilini au una mikwaruzo.
- Unaweza kuota unafanya mapenzi na watu au wanyama
- Unaweza ota unalima na asubuhi unaamka umechoka
- Unaweza kuhisi mwili wako kuna vtu vinatembea kama siafu au joto lisilo la kawaida sehemu ya viungo
- Kuhisi ganzi na kichwa upande mmoja kisichopona
- Macho kushindwa kuona darasani au ofisini lakini ukiwa nje unakuwa sawa
- Kushindwa tendo la ndoa au kuhisi hupendi kabisa na ukilazimisha unashindwa
- Kupiga mihayo mingi mara kwa mara bila usingizi au njaa
- Kuhisi umebeba vitu mgongoni na kuhisi kifua kizito
- Kuhisi kuna mtu amekusimamia au anakufuata nyuma na ukigeuka huoni mtu huyo
- Kukata tamaa ya maisha na kuona kila kitu hakiwezekani
- Kuingia kwenye hedhi bila mpngilio na kwa shida
- Kutoka damu ya hedhi bila kukoma kwa miezi au damu kupotea na hali huna mimba
- Kuchukiwa na kila mtu bila sababu hata jamaa na marafiki
- Kuongea usiku na kupiga kelele
- Kuota nyoka mara kwa mara na paka hasa weusi
- Kuota uko msituni mara kwa mara
- Kuota uko chooni au bafuni au sehemu chafu mara kwa mara
- Kuota unakojoa mara kwa mara na wakati mwingine unakaribia kukojoa kitandani
- Kuota watu waliokufa na unaongea jamaa zako marehemu mara kwa mara
- Kuota uko makaburini mara kwa mara
- Choo
inakuwa ngumu hata kama unakula matunda na unajisaidia mavi kama ya
mbuzi kwa taabu na muda wote na hili hali minyoo hauna baada ukipima
choo.
- Kutingishika baadhi ya viungo vya mwili na kuhisi kitu kinatembea tumboni mgongoni au sehemu za mwili
- Kuota unagombana na kundi la watu kwa vitisho mpaka unatoka jasho
- Kuhisi woga na moyo kudunda mara kwa mara ghaflaukitoka usingizini au ukiwa peke yako
- Mipango yote muhimu kuwa inavurugika ikikaribia kuwa sawa
- Kshindwa kuoa au kuolewa na ukipata mchumba mara mipango inaharibika mwishoni
- Kuota unakufa na unazikwa
- Kuwa mzembe na kupenda kulala sana wakati mwingine saa nne ndo unapenda kuamka
- Bosi
kukuchukia bila sababu na ukiongea hataki wala mawazo yake ila ni
kukufokea hata ujitahidi kuwa mpole na mchapa kazi wa hali ya juu
- Kuona mme au mke anayo sura ya ajabu kama ya nguruwe au mbwa na hili hali wengine wanamuona mzuri
Dalili hizo ni za kufanyiwa uchawi au kuwa na majini yanayokusumbua ya kiuchawi
Kuna tatizo hili sana hasa mtu akiwa amevalishwa nguvu za giza na
hata akiwa anafanyiwa mazingira ya kuhujumiwa kwa nguvu za kishirikina.
Tiba
yake ni kuwa unajipaka mafuta haya Powerful Oil na hii itafukuza nguvu
za giza na negative energies zote zitaondoka na utahisi mwepesi na
mwenye akili nzuri za kutafakari.
Unajipaka usoni, kifuani na
kichwani kila siku mpaka unaposikia umekuwa sawa hasa siku saba utaanza
kuwa sawa kwa uwezo wa Mungu uliopo ndani ya mafuta haya na miti
iliyotoa mafuta na dawa zilizomo.
Dawa nyingine za kunywa ni hizi:
MT32-Magonjwa mengi mwilini na hasa uchawi wa kuwekwa mwili na
jini vikawa vinatembea kwenye mishipa ya damu mpaka unahisi kitu au
vitu vinatembea mwilini kwa ndani hasa mgongoni na mabegani kama vijiwe
au panya anatembea kwa pozi la aina yake.
SAFISHA-unaharisha uchawi na kuondoa visivyotakiwa kiafya
tumboni na hii inasaidia kusafisha utumpo na mishipa muhimu ya kutoka
tumboni
Madawa haya yanatokana na mitishamba mbali mbali ya Africa na
Mashariki ya Kati na yanatibu magonjwa mengi unayo yajua na yale
usiyojua. Madawa haya ni unga umesagwa na ni rahisi kutumia kwenye maji
moto au asali na hakuna kemikali yoyote. Powerful oil ni mafuta yenye
uwezo mkubwa wa kufukuza na kuzuia nguvu za giza za aina zote.
Ukiwa
umepima hospitali na hauponi basi tafuta tiba za kutibu uchawi kuondoka
mwilini na kuondoa majini kwa maombi sahihi na madawa ya kunywa na
kujipaka ili mashetani yaondoke mara moja kwa uwezo wa Mungu mmoja wa
pekee.
Mawasiliano: Upate huduma